Maneno

Rebekah Dawn

Added on : Nov 28, 2017

Maneno – Rebekah Dawn
Nov 28, 2017 Oluwasetemi
In Lyrics

Wakati mwingine nikiketi kukuimbia mie
Huwa nalemewa kupata maneno yanayoshimiri
Ni kama mtoto mchanga anapojaribu kueleza ukubwa wa sayari
Ni kama kidege kinapojaribu kueleza upana wa mbingu
Ni kama changarawe kujaribu kueleza ukubwa wa bahari

Ukweli ni kwamba maneno yangu hayatoshi, hayawezi kueleza
Hivyo daima na milele siku zote za maisha yangu
Nitatafuta kukuimbia maneno yanaykufaa

Wakati mwingine nikiketi kukuimbia mie
Huwa nalemewa kupata maneno yanayoshimiri
Ni kama tone la maji kujaribu kueleza mfuriko wa mvua
Ni kama wapendanao kujaribu kueleza fumbo la penzi
Ni kama mshumaa kujaribu kueleza kung’aa kwa jua

Ukweli ni kwamba maneno yangu hayatoshi, hayawezi kueleza
Hivyo daima na milele siku zote za maisha yangu
Nitatafuta kukuimbia maneno yanaykuofaa

Ni kama jiwe linapojaribu kueleza urefu wa mlima
Ni kama sheha shupavu kujaribu kueleza hadithi zote za jadi
Ni kama mwenye dhambi kujaribu kueleza neema ya msamaha

Ukweli ni kwamba maneno yangu hayatoshi, hayawezi kueleza
Hivyo daima na milele siku zote za maisha yangu
Nitatafuta kukuimbia, nitatafuta kukuimbia
Maneno yanaykuofaa

HOW HAS THIS IMPACTED YOUR LIFE?

Thank you for sharing. Show us some love by joining our community.

Send this to a friend